April 26, 2013






Sare ya mabao 1-1 kati ya Coastal Union na Azam FC imeipa Yanga ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Yanga imekuwa bingwa kwa kufikisha pointi 56 ambazo tayari ilikuwa nazo na Azam FC ndiyo ilionekana kuiopa presha.


Lakini sare hiyo ya leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga imeiruhusu Yanga kubeba taji hilo kwa kuwa Azam haiwezi kufikia.

Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ameiambia Salehjembe kuwa ubingwa huo mapema wakiwa na mechi mbili mkononi ni matokeo ya kazi na umoja.

“Mkishirikiana siku ya mwisho mnapata matunda bora, ushindi umekuja tukiwa hatuchezi na tumepumzika.

“Hayo ni matokeo ya kujituma lakini bado nitafurahi tukishinda mechi mbili zilizobaki dhidi ya Coastal Union na Simba,” alisema Brandts raia wa Uholanzi.

Katika mechi hiyo ya Mkwakwani, Azam walitangulia kufungwa kwa mkwaju wa penalty kupitia kwa beki wake Agrey Morris lakini Coastal wakasawazisha kupitia Daniel Lyanga aliyekuwa ameingia kipi cha pili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic