May 2, 2013


Cheka..


Bondia Francis Cheka ameonyesha hana mpinzani katika masumbwi katika kipindi hiki baada ya kumchapa Thomas Mashali.

Cheka kamchapa Mashali katika raundi ya 10 katika pambano lao la raundi 12 lililomalizika muda mchache uliopita kwenye Ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam.
 
Mashali..
Ingawa Mashari alionyesha ushindani mkubwa kuanzia raundi za mwanzo, kadri muda ulivyokuwa unasonga mbele alishindwa kuhimili vishindo vya bondia huyo wa Morogoro.

Raundi ya 10, Cheka alimtwanga konde lililompeleka Mashali ambaye aliona bora shari kamili na kuamua kukubali kwamba amekwisha.
Kutokana na ushindi huo, Cheka amebeba gari aina ya Toyota Noah ambayo mshindi wa pambano hilo aliahidiwa.

Awali Mashali alikuwa akitamba kwamba yeye ndiye bondia pekee anayeweza kumchapa Cheka baada ya kuwashinda karibu mabondia wote wanaojulikana nchini kwa kuwa na uwezo mkubwa.

Lakini imeshindikana na sasa imethibitika kwamba Cheka, hana mpinzani nchini hasa baada ya kuwapiga lundo la mabondia wakiwemo wakali kama akina Rashid na Hassan Matumla, Maneno Oswald ‘Mtambo wa Gongo’, Karama Nyilawila na wengine kibao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic