May 2, 2013


Igboananike


Ukitaka kujua Wanigeria au wachezaji kutoka Afrika Magharibi hupania kupata mafanikio wanapopata timu za kucheza soka la kulipa barani Ulaya tofauti na wale wanaotokea Tanzania, Kennedy Igboananike anaweza kuwa mfano.
 
Machuppa..
Igboananike raia wa Nigeria sasa amenunuliwa na AIK Stockholm, moja ya klabu kubwa nchini Sweden na sasa atakuwa akilamba mshahara wa zaidi ya Sh milioni 10 za Tanzania.
 
Igboananike
Igboananike  aliyezaliwa Februari 26, 1989 jijini Lagos, Nigeria, aliwahi kucheza kikosi kimoja cha Vasalund ya daraja la kwanza na Mtanzania, Athumani Machuppa.
 
Igboananike wakati akicheza Vasalund..
Wakiwa pamoja, Igboananike  alikuwa analazimika kukaa benchi ili kumpa nafasi Mtanzania huyo acheze, lakini sasa Igboananike amepiga hatua kubwa na kununuliwa na klabu hiyo.

Kununuliwa na klabu hiyo kubwa ni dalili kwamba Igboananike anaweza kupata timu nzuri zaidi katika nchi zinazolipa kama Italia, Ujerumani, Hispania au England.

Lakini Machuppa anaelekea kustaafu na mwisho wake katika klabu ya Vasalund haukuwa mzuri sana. Taarifa zinaeleza yuko nchini, haijajulikana kama ameamua kuachana na soka au atapumzika hadi msimu ujao.

Salehjembe inaendelea kujaribu kufanya naye mawasiliano ili kutaka kujua mpango wake kwa kuwa alipotua Sweden alikuwa mmoja wa washambuliaji wanaokubali ndiyo maana Wanigeria kama Igboananike  walilazimika kusubiri.

Igboananike  alitua Sweden mwaka 2008 na kujiunga na Vasalunds IF ambako alicheza mismu miwili mwaka 2009 Machuppa alipokuja Vasalunds if aliwekwa benchi. Mishoni wa msimu 2010 akanunuliwa na Djurgåden timu kubwa ya premier alikaa misimu miwili mpaka mwaka jana ametula zaidi kwa kujiunga na AIK Stocholm.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic