May 2, 2013



Cheka mdogo akishangilia baada ya kutangazwa mshindi dhidi ya Mashali mdogo...


Wakati mashabiki walikuwa wanasubiri kwa hamu pambano la Francis Cheka dhidi ya Thomas Mashali, wadogo zao nao walipewa nafasi katika pambano la utangulizi.


Cosmas Cheka kutoka Morogoro dhidi ya Charles Mashali wa Manzese jijini Dar nao walionyesha kazi.

Pambano lao la raundi nane lilikuwa la kuvutia na madogo hao walichapana makonde vilivyo.


Kila mmoja alionyesha kumpania mwenzake, walikuwa wakipelekana kwenye kona na kushambuliana mfululizo.


Kijana Francis anayetokea katika kambi ya kaka yake, Cheka mwisho aliibuka na ushindi na wazi ikaonyesha ni utabiri mzuri wa pambano litakalofuata la kaka zao.

Kweli, ndivyo ilivyokuwa baada ya Cheka kumchapa Mashali kwa KO katika raundi ya kumi na kumaliza mchezo kabisa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic