May 2, 2013



Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limetaka kuanzwa upya kwa utaritibu wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa Shirikisho la Sika Tanzania (TFF).


Uamuzi huo wa Fifa, maana yake mchakato huo utaanza upya na unawaruhusu wote walioondolewa awali kama Jamal Malinzi na Michael Wambura kuwa huru kugombea tena.

Pamoja na hivyo Fifa imeitaka TFF kuanzisha chombo kitakachoitwa kamati ya maadili na hadhi kwa ajili ya kusimamia mchakato huo.

Awali Fifa ilizuia uchaguzi huo ambao ulipangwa kufanyika Februari, mwaka huu, baada ya kukumbwa na migogoro, lakini baada ya kufanya mahojiano na shirikisho hilo, wagombea pamoja na kamati mbalimbali (Fifa) wametoa maagizo hayo.


Akizungumza na waandishi wa habari hivi punde, Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema Fifa wamewaeleza kuna kasoro kati zilizojitokeza huku wakisisitiza kuundwa kwa kamati ya maadili na hadhi kabla ya Oktoba, mwaka huu.

 “Fifa wamesema kuwa kuna sehemu tulikuwa tunakosea, tunatakiwa kuunda kamati ya maadili na hadhi ambayo itakuwa na mwanasheria ndiyo tuweze kuendesha uchaguzi huu.

“Wamepatupa muda hadi Oktoba na mchakato wote unaanza upya, wanaotaka watalipia fomu upya na kila kitu kwa sasa kitakuwa kipya kabisa,” alisema Tenga.

“Kwa kuwa mchakato utaanza mapema, Fifa wameomba tutengeneze taarifa ya mambo yanavyokwenda kabla ya Oktoba ili kuokoa muda kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.”


Maana yake, Tenga aliyekuwa amemaliza muda wake zaidi ya miezi mitano iliyopita, ataendelea kuula katika nafasi hiyo akishughulikia maandalizi ya uchaguzi.

Uamuzi wa Fifa kuunda kamati hiyo, unaonyesha umelenga kufanyika kwa mchakato upya, lakini bado inaonekana kutakuwa na ugumu kwa baadhi ya wagombea kama suala lao litafikishwa katika kamati hiyo ya hadhi na maadili itakayokuwa imeundwa na TFF.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic