May 3, 2013




Na Mwandishi Wetu
MLEZI wa Simba, Rahma Al Kharusi amevunja ukimya wa muda mrefu na kusema anaendelea kufanya shughuli za klabu hiyo kwa kuwa sasa yuko nchini England.

Rahma maarufu kama Malkia wa nyuki amesema yuko jijini London kwa ajili ya mkutano maalum na mmiliki wa Sunderland, Ellis Short kujadili mambo kadhaa kwa faida ya klabu hizo na hasa Simba.
 
Ellis Short..
Short ndiye mmiliki wa klabu ya Sunderland na aliyempa kazi kocha matata Muitaliano, Roberto Di Canio ambaye ana kibarua kigumu cha kuikoa timu hiyo isiteremke daraja baada ya kukumbana na kipigo cha mabao 6-1 kutoka kwa Aston Villa, wiki iliyopita.

“Nipo, kama nilivyosema awali, zaidi nimewekeza nguvu zangu kwa ajili ya msimu ujao. Sasa niko London na baadaye nitaenda Sunderland kwa ajili ya kukutana na mmiliki wake.

“Kuna masuala kadhaa ya msingi kuhusiana na uhusiano mpya wa Simba na Sunderland, najua Simba ndiyo itafaidika zaidi.

“Ratiba ni kwamba nitakutana na watu wa Sunderland na ratiba yao na mimi itakuwa kuanzia Jumapili hadi Jumanne,” alisema Malkia we nyuki.

Taarifa zinaeleza huenda Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage naye akaungana na Malkia wa Nyuki nchini humo ndani ya leo na kesho.

Akiwa jijini Dar es Salaam mwezi uliopita, Malkia wa nyuki alizungumza na Short kuhusiana na suala la uhusiano wa klabu hizo mbili na mmiliki huyo bilionea wa Sunderland akatoa mwaliko huo.

Iwapo Simba itafanikiwa kuingia mikataba ya kimaendeleo na Sunderland yenyewe ndiyo itafaidika zaidi kwa kuwa Waingereza hao wamepiga hatua zaidi kimaendeleo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic