May 3, 2013




Baada ya mzunguko wa muda mrefu, hatimaye kipa wa Yaw Berko amemalizana na uongozi wa klabu hiyo.

Tayari Berko yuko tayari kuondoka na kuendelea na maisha yake baada ya Yanga kumlipa haki zake.

Berko raia wa Ghana aliondolewa katika kikosi cha Yanga kwa madai ya kuwa na maringo hali iliyofanya uongozi wa Yanga uone hajitoi asilimia mia kwa ajili ya klabu hiyo.


Ikaamua kumpeleka kwa mkopo katika timu ya DC Motema Pembe ya DR Congo ambako baadaye hawakuelewana akaamua kurejea nchini.

Baada ya kurejea, alikuwa akiishi katika makao makuu ya klabu hiyo kwa kujificha huku ikionyesha wazi hakutaka kuonekana.

Berko alikataa kuzungumzia suala lake, lakini mmoja wa viongozi wa Yanga, hakutaka kutajwa mtandaoni alisema Berko ameshalipwa stahiki zake.

“Ataondoka hivi karibuni, ameshalipwa haki zake na kuna mambo kidogo tu ya kukamilisha,” alisema.

Salehjembe inaendelea kumsaka Berko ili kujua undani wa suala hilo na ataondoka lini kuelekea wapi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic