May 19, 2013


Mashabiki Yanga wakimzungusha Ngassa uwanjani mara baada ya mechi dhidi ya Simba kwisha jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Hatimaye Kiungo mwenye kasi, Mrisho Khalfan Ngassa amefunguka na kusema amesaini Yanga mkataba wa miaka miwili.

Salehjembe ilikuwa ya kwanza kuandika kuhusiana na Ngassa kusaini Yanga katika mitandao.

Ngassa amezungumza kwa mara ya kwanza na kuthibitisha kwamba kweli amesaini Yanga.


“Ni kweli nimesaini Yanga, nisingeweza kuzungumzia suala hilo wakati nina mkataba ambao ulikuwa haujamalizika.

“Lakini baada ya mechi ya mwisho ya ligi, sasa niko huru kuanza kuutumikia mkataba wangu mpya,” alisema.

Mashabiki wa Yanga walimchukua Ngassa na kumvisha jezi ya njano na kijani, mara tu baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Yanga na Simba kwenye Uwanja wa Taifa, jana.

Mashabiki hao walimvisha jezi hiyo na kumbeba na kumbeba na kuondoka naye hadi nje ya uwanja.
 
Azam FC ilimpeleka Simba kwa mkopo, lakini Simba imekuwa ikisema ilimuongezea mkataba wa mwaka mmoja na kumlipa Sh milioni 30 pamoja na gari.

Lakini Ngassa mwenye amekuwa akisisitiza kuwa hana mkataba na Simba kama ambavyo Wekundu hao wa Msimbazi wamekuwa wakitangaza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic