May 19, 2013





Pazia la Ligi England limefungwa leo huku vita ya nafasi ya tatu na nne ikipata wenyewe.

Chelsea imefanikiwa kushika nafasi ya tatu baada ya kuichapa Everton kwa mabao 2-1 na kufikisha point 75.


Wakati Arsenal iliyokuwa inachuana kwa nguvu na Tottenham, imefanikiwa kupata nafasi ya nne kwa kuichapa Newcastle kwa bao 1-0 na kufikisha pointi  73.

Pamoja na Spurs kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Sunderland, imejikuta ikianguka nafasi ya tano kutokana na kuwa na pointi 72, kitu ambacho kimezua majonzi katika kikosi hicho cha London.


Tayari nafasi ya kwanza ilikuwa na wenyewe Man United ambao mabingwa hao wamemaliza mechi yao dhidi ya Wes Brom kwa sare ya ‘netiboli’ ya mabao 5-5.


Man City waliokuwa wamejihakikishia nafasi ya pili walilala dhidi ya Norwich kwa mabao 2-3 wakiwa nyumbani Etihad.


Mechi nyingine, West Ham ikaichapa Reading 4-2, Swansea ikalala kwa mabao 3-0 dhidi ya Fulham, Liverpool ikaichapa QPR 1-0.

Southampton ikawa 1-1 dhidi ya Stoke, Wigan na Aston Villa wakamaliza na sare ya 2-2.



Teams
P
GD
PTS
1
38
43
89
2
38
32
78
3
38
36
75
4
38
35
73
5
38
20
72

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic