May 1, 2013



Pamoja na kutokuwa katika presha ya kutoteremka daraja au kubeba ubingwa, Ruvu Shooting imepanga kuichapa Simba katika mechi yao ya Ligi Kuu Bara itakayopigwa Mei 5, kwenye uwanja wa Taifa, Dar.

Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amesema wamejiandaa vilivyo na wanazitaka pointi tatu za Simba.


Ruvu Shooting inayofundishwa na kocha mkongwe, Charles Boniface Mkwasa imekuwa ni kati ya timu zinazoonyesha soka la kuvutia.

Tayari iko katika nafasi ya saba ikiwa na pointi 30 ambazo zinaiweka katika nafasi ya kutokuwa na hofu ya kuteremka daraja.

 “Mazoezi yanaendelea, naweza kusema kama mandalizi tunajua Simba ni timu ngumu na wanataka nafasi ya tatu, lakini wasitegemee kutugeuza njia. Sisi pia tunataka pointi tatu,” alisema Masau.

Ruvu Shooting imekuwa ni kati ya timu zinazoisumbua Simba zinapokutana lakini Mfaransa wa Simba, Patrick Liewig amesisitiza wanataka kushinda mechi mbili dhidi ya timu hiyo ya jeshi na ile dhidi ya watani wao Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic