May 1, 2013




Beki wa kati wa Yang, Mbogo Ladslaus yuko fiti na anaweza akacheza mechi mbili za Ligi Kuu Bara ambazo Yanga imebakiza.

Mechi hizo ni ile ya leo dhidi ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa na ile ya Mei 18 dhidi ya watani wao Simba.


Daktari wa Yanga, Nassor Matuzya amesema tayari amemkabidhi Mbogo kwa Kocha Mkuu, Ernie Brandts ambaye ataamua kama atampanga au la.

“Sasa Mbogo yuko fiti na anaweza kucheza, nimeshazungumza na kocha. Hivyo ndiye mwenye uamuzi wa mwisho kama acheze au la,” alisema.
Beki huyo wa kati aliyejiunga na Simba akitokea Toto African alifanyiwa upasuaji huo katika Hospitali ya Mwananyamala ambayo alilazimika kukaa nje ya uwanja kwa zaidi ya mwezi.

Wiki moja iliyopita alirejea na kuanza mazoezi na wenzake hadi jana Matuzya aliposema yuko fiti na anaweza akacheza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic