May 19, 2013

Mashabiki wa Man City wameonyesha kuumizwa na uamuzi wa kocha wao wa zamani, Roberto Mancini kulipia tangazo kwa ajili ya kuwaaga.

Tangazo hilo la kwenye gazeti la Manchester Evening lilipiwa na Mancini na kuandika ujumbe, “miaka mitatu isiyosahaulika, sitawasahau mashabiki wa Manchester City. Milele mtabaki moyoni mwangu.”

Halafu kuna picha ya mashabiki, Mancini na ngao ya hisani, makombe ya Ligi Kuu England na FA.

Mashabiki waliohojiwa na televisheni ya Sky wamesema alichofanya Mancini ni kitu cha aina yake na imewaumiza kutokana na uungwana kupindukia ambao haujawahi kufanywa na kocha yoyote nchini humo.

Mancini alitupiwa virago baada ya timu yake kushika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Man United na Manuel Pellegrin ndiye anaelezwa kuja kuchukua nafasi yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic