June 7, 2013

 


Klabu ya Reading imefanikiwa kuwazidi QPR kwa kufanikiwa kumsajili beki wa kushoto wa Manchester City, Wayne Bridge.

Bridge mwenye umri wa miaka 32 ambaye aliwahi kukwakuruzana na John Terry wa Chelsea kutokana na Terry kufanya ngono na aliyekuwa mpenzi wa mchezaji huyo, amekuwa huru baada ya mkataba wake na Man City uliomwezesha kuvuna pauni 90,000 kila wiki kumalizika.

Bridge amekuwa akitumia muda mwingi akiwa nje ya Man City lakini aligoma kuvunja mkataba wake, hivyo licha ya kupelekwa timu nyingine kwa mkopo au kuwepo klabuni hapo huku akiwa hachezi, bado aliendelea kupata mshahara wake kama kawaida.

Nina furaha kujiunga Reading naimani nimefanya chaguo sahihi,” alisema Bridge na kuongeza:

“Nimezungumza na kocha na amenielekeza nia yake ya kule timu anapotaka timu ielekee, amefurahishwa sana na usajili wangu hapo.”

Kutokana na mvutano huo, Bridge aligoma kumsalimia Terry kwa kutompa mkono wakati Man City na Chelsea zilipokutana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic