June 10, 2013


Thiago akiwa na Neymar ambaye tayari ametua Barca..


Tayari Barcelona wameanya kazi ya kuhakikisha wanapata mrithi wa beki wao mkongwe, Carles Puyol ambaye umri na majeruhi vimepunguza uwezo wake.
 
Kompany akimdhibiti Torres wa Chelsea...
Barcelona imepanga majina ya mabeki tisa kutoka timu mbalimbali za Ulaya ingawa chaguo la kwanza linaonekana kuwa ni Thiago Silva wa PSG.


Pamoja na Thiago, Barcelona pia imewalenga Hummels (Dortmund), Kompany na Lescott (City), Marquinhos (Roma), David Luiz and Ivanovic (Chelsea), Ínigo Martínez (Real Sociedad) na Vermaelen (Arsenal).

Lengo la Barcelona ni kuwa na beki imara kwa kuwa msimu uliopita, safu yake ya ulinzi ilionekana kuyumba, kitu ambacho hawataki kitokee msimu ujao.

Suala la Thiago ambaye amepewa nafasi ya kwanza na Kocha Mkuu, Tito Vilanova litategemea bei kutoka kwa PSG, kama itakuwa juu sana, basi Barcelona wataanza kuangalia mabeki wengine kwa kufuata listi yao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic