June 10, 2013




Kocha Carlo Ancelotti ameonyesha kukerwa na tabia ya uongozi wa PSG kuonyesha unataka kumbakiza.

Ancelotti raia wa Italia amemuambia rafiki yake wa karibu aliyezungumza na gazeti la Le Parisien la Ufaransa kwamba anataka kwenda Madrid lakini PSG wanaonekana kutaka kumlazimisha kubaki.

Kocha huyo wa zamani wa AC Milan na Chelsea amesema Rais wa PSG, Nasser Al Khelaifi amekuwa akitaka kulazimisha abaki lakini yeye anataka kuondoka.


Rafiki yake huyo amesemma tayari Ancelotti ameshafuta mawazo ya kubaki PGS na anataka kuendelea mbele na Madrid ndiyo ndoto yake kwa kuwa pia inamhitaji kuchukua nafasi ya Jose Mourinho aliyerejea Chelsea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic