June 18, 2013


Mtanzania Yona Ndabila amekumbana na balaa kwa kulambwa kadi nyekundu ikiwa ni mechi nne tu baada ya kuichezea timu yake mpya.

Ndabila awali alikuwa akiichezea Saraswoti Youth Club kwa takribani misimu mitatu kabla ya kujiunga na Manang FC ambayo ni moja ya timu kubwa nchini Nepal



“Kweli nimepigwa kadi nyekundu, sikutegemea na ilikuwa ni hali ya kawaida tu ya mchezo lakini huenda mwamuzi hakuelewa.

“Lakini hakuna kitu kibaya, naendelea kupambana kwa ajili ya kuhakikisha naisaidia timu yangu. Kipindi nitakachokuwa nje kutokana na adhabu hiyo nitaendelea na mazoezi kwa juhudi,” alisema Ndabila.

Akiwa nchini Ndabila aliwahi kung’ara na Prisons ya Mbeya pamoja na Mtibwa Sugar ya Morogoro lakini baadaye aliamua kutoka nchini na kwenda nje kutafuta maisha.


Wakati akicheza soka nchini, Ndabila aliwahi kuwa mmoja wa wachezaji waliokuwa katika kikosi cha Stars chini ya Marcio Maximo ambacho kilisafiri na kwenda kucheza mechi ya kirafiki nchini yemen.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic