June 10, 2013


Mshambuliaji Edinson Cavani ameweka wazi kwamba angependa kufundishwa na makocha wawili.
Cavani raia wa Uruguay amewataja makocha hao kuwa ni Jose Mourinho au Manuel Pellegrini.
Maana yake, Cavani amechagua kuhamia Ligi Kuu England kwa kuwa makocha hao wote watakuwa England.
Mourinho ameishatua Chelsea na Pellegrini anaonekana kuwa mali ya Manchester City.

“Bado nina mkataba na Napoli, lakini ninazungumza na klabu nyingine, makocha hao wawili ningependa kufanya kazi na mmoja wao,” alisema.

Alipoulizwa kuhusiana na Real Madrid, akajibu, “sina uhakika, kila mtu angependa kucheza La Liga, lakini bado sijajua mwisho wangu.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic