June 10, 2013

Siku moja tu baada ya kiungo nyota wa Barcelona, Andres Iniesta kutamka kwamba Kocha Jose Mourinho alichangia kuua soka la Hispania, kocha huyo amejibu.
Mourinho aliyekuwa kocha mkuu wa Real Madrid amesema anakubaliana na Iniesta kwamba aliua soka la Hispania kwa kuwa alivuruga tabia za Barcelona kuwa timu isiyofungika.
“Kweli kama kuondoa utawala wa Barcelona kuwa timu isiyowezekana ni kuua soka la Hispania, basi yuko sahihi.


“Kwa mtu anayefuatilia atakuwa na majibu, kwamba Barcelona ilionekana ni timu isiyofungika na walijua kila kitu.
“Hata mimi mwanzo nilifungwa mabao matano, lakini nilituliza akili na kujipanga, baadaye waulize, kazi yangu wanaijua hivyo kama hivyo ni kuua soka, basi sawa.”
Jana Iniesta alimshambulia Mourinho na kusema amevuruga na kuporomosha soka la Hispania, lakini bado ilionekana pia kauli yake ililenga kumtetea rafiki yake Iker Casillas aliyekuwa na ugomvi mkubwa na Mourinho.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic