June 18, 2013




Wachezaji nyota wa timu ya taifa ya Ufaransa, Frank Riberry na Karim Benzema wamefikishwa kizimbani kutokana na kupata huduma ya changudoa mwenye umri mdogo.


Changudoa huyo aitwaye Dehar mwenye asili ya Algeria amesema wachezaji hao walijua ana umri mdogo lakini bado walikubali kupata huduma yake.

Imeelezwa Riberry ambaye anakipiga Bayern Munich alipata huduma ya Dehar wakati akiwa na miaka 17.


Dehar ameileza mahakama kuwa Riberry alimlipia ndege na kumsafirisha hadi Munich ambako kulikuwa na sherehe yake ya kuzaliwa na ‘akamtumia’ mwisho akampa ujira wa euro 700 tu.


Lakini changudoa huyo dogodogo amesisitiza hata Benzema anayekipiga Real Madrid alimtumia pia wakati akiwa na miaka 16 huku akijua ni makosa.

Wote wawili wamekanusha ingawa Riberry amesema amewahi kumjua Dehar na aliwahi pia kumlipia euro 200 kwa ajili ya taxi na si zaidi.

Wachezaji hao nyota hawakutokea mahakamani na badala yake waliwakilishwa na wanasheria wao.

Kwa mujibu wa sheria za Ufaransa, iwapo watapatikana na hatia, basi watahukumiwa kwenda jela miaka mitatu au faini ya euro 40,000.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic