June 18, 2013




Pamoja na kuwa msumari wa moto kwa mabeki wa Tanzania, mshambuliaji wa Arsenal, Gervinho amezua gumzo kutokana na tabia yake ya kukosa mabao ya wazi.

Mashabiki wengi wa Arsenal wamekuwa wakilaumu kuhusiana na mchezaji huyo kupoteza nafasi za wazi katika mechi za Ligi Kuu England.


Katika mechi ya juzi dhidi ya Taifa Stars, Gervinho alikuwa moto wa kuotea mbali wakati akiichezea Ivory Coast kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Lakini moja ya kitu alichofanya na kusababisha mjadala huo ni kukosa bao la wazi akiwa amebaki yeye na kipa Juma Kaseja.


Gervinho aliwazidi mbio mabeki wa Stars, Nadir Haroub Cannavaro na Kelvin Yondani, baada ya kubaki na Kaseja, alipiga mpira dhaifu ambao ulikwenda moja kwa moja kwenye mikono ya kipa huyo.

Ingawa wengi walifurahi kutokana na kukosa kwake, lakini mashabiki wengi wa soka la England walianza kumjadili.

Katika baadhi ya mitandao wamemuelezea kama mchezaji hatari katika suala la kusumbua na kupiga krosi lakini si kufunga.

Gervinho ni kati ya wachezaji wanaopoteza nafasi nyingi sana za kufunga akiwa katika nafasi nzuri ya kufanya hivyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic