| PICHA NAMBA MOJA |
| PICHA NAMBA MBILI |
Na Saleh
Ally
BADO
naendelea kusisitiza, kikosi chetu cha Taifa Stars kilifanya kila
kinachowezekana kadri ya uwezo wake lakini ndiyo hivyo, mwisho wa mchezo kikawa
kimelala kwa mabao 4-2 dhidi ya wababe Ivory Coast.
Kila mmoja
ambaye alifanya juhudi zake kuhakikisha anaona Stars inaibuka na mchezo huo
anastahili pongezi, mashabiki ni sehemu ya walioonyesha uzalendo wa dhati.
Lakini kila
kosa lazima liwe msaada, nikimaanisha kila unapokosea ni lazima kujifunza kwa
ajili ya kusaidia mambo hapo baadaye.
Ukiangalia
mechi hiyo ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia kati ya Taifa Stars na
Ivory Coast kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumapili iliyopita,
utagundua hakuna tofauti kubwa ya soka.
Lakini
Ivory Coast walionyesha walijua wanachofanya na mambo mengi waliyopanga
yalikwenda kama walivyopanga. Kosa kubwa zaidi kwao ni bao la kwanza la Stars
alilofunga Amri Kiemba, walijisahau wakashindwa kufunga.
Kosa hilo
likahamia Stars na utaona picha katika ukurasa huu zinaonyesha tofauti kubwa
kati ya Ivory Coast na Taifa Stars hasa katika suala la ukabaji ‘marking’.
Bao la kwanza:
Ukiangalia
bao la kwanza walilofungwa Stars, utaona wachezaji wawili wa Ivory Coast (Yaya
Toure na Lacina Traore wakiwa katika boksi ya 18 na wachezaji wanne wa Taifa
Stars ambao ni Salum Abubakari ‘Sure Boy’, Frank Domayo, Kelvin Yondani na
Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Ajabu
hakuna hata mchezaji mmoja wa Stars ambaye alikuwa amemkaba Yaya au Traore,
ndiyo maana mara baada ya Gervinho kutoa pasi kwa Toure, wakati Cannavaro
anamfuata, mara moja akatoa pasi kwa Traore ambaye pia alikuwa peke yake,
akapachika bao kilahisi kabisa. (Angalia picha 1&2).
Bao la nne:
Mabao
mengine mawili yalikuwa ya penalti na lile la faulo. Lakini ukiangalia bao la
nne pia, baada ya Gervinho kumtoka Erasto Nyoni na kupiga krosi iliyoguswa na
Kaseja, wachezaji wote wa Stars walikuwa upande mmoja.
Hata kama
mpira uliguswa, kama ‘marking’ ingekuwa makini, hapa shaka mabeki ndiyo
wangekuwa wa kwanza kuuwahi. Kama mambo yangeenda kwa mpangilio, hata baada ya
Kaseja kuuguza ule mpira, basi beki mmoja tu angepotea.
Kitendo cha
mabeki wote kwenda kucheza mpira mmoja huku wachezaji wawili wa Ivory Coast,
Yaya na Bonny Wilfried kuwa ‘free’ ikawa
ni lahisi kwao kufunga kwani hata angeukosa mfungaji basi ule mpira ungeenda
kwa Yaya ambaye pia angefunga.
Umakini:
Angalia
Ivory Coast walivyokuwa makini katika suala la ulinzi, huenda ingekuwa bora
zaidi kama Stars wangefanya hivyo. Angalia picha namba tatu inaonyesha Thomas
Ulimwengu akiwa ameruka katika msitu wa mabeki watano wa Ivory Coast, huo ndiyo
ulinzi.
Lakini
angalia namna kipa wa Stars, Kaseja akiwa ameruka kuda mpira kwenye msitu wa
wachezaji wa Ivory Coast lakini hatua kama nne au tano hauoni hata beki mmoja
aliye tayari kumsaidia.
Bado
angalia picha namba nne, faulo imechongwa ndani ya lango la Ivory Coast, mabeki
wao wawili wameruka pamoja na kipa kumthibiti mchezaji mmoja wa Stars.
Lakini
ukiangalia wachezaji wengine wa Stars kila mmoja amethibitiwa. Didier Zokora
amemkumbatia Mbwana Samatta na Souleman Bamba amemkumbatia Kiemba. Kwa kifupi
hawajawapa nafasi hata kama mpira utamtoka kipa, wako karibu hao kuokoa.
Lakini
angalia picha namba tano ambayo Kaseja ameruka na kudaka mpira ndani yam situ
wa wachezaji wanne wa Ivory Coast na hakuna aliye karibu kusaidia iwapo
atafanya kosa kama binadamu.
Hili ni
somo kubwa, huenda soka Stars haikuzidiwa sana. Lakini ujuzi zaidi, umakini
unaotakiwa ndiyo uliwangusha kwa kuwa walikosa siku hiyo. Hivyo Kocha Kim
Poulsen inabidi ayafanyie kazi haya.
Si lahisi
timu ikawa inafunga halafu lahisi kufungwa, ndiyo maana ugumu ulionekana siku
hiyo na Ivory Coast wakayatumia makosa hayo kuiangusha Stars.







0 COMMENTS:
Post a Comment