June 11, 2013


Kocha mpya wa Chelsea, Jose Mourinho amesema yuko tayari kufanya kazi na mshambuliaji Wayne Rooney.


Mourinho amesema Rooney ni kati ya wachezaji wanaomvutia na milango iko wazi kama atakuwa tayari kufanya naye kazi Stamford Bridge maarufu kama darajani.

Rooney amekuwa hana raha siku chache baada ya Ferguson kustaafu soka kwa kuwa walikuwa wamelumbana.

Lakini kutua kwa David Moyes ambaye ni kocha wake wa kwanza akiwa Everton pia kunaonyesha hatakuwa na furaha kubaki Man United kwa kuwa waliwahi kulumbana wakati wakiwa wote.

Hata hivyo, Chelsea iko katika vita ya kuhakikisha inamnasa mshambuliaji Edinson Cavani wa Lazio.


Rooney ni mzaliwa wa Liverpool ambako alichupukia akicheza soka ambako alijiunga na timu ya watoto ya Everton baada ya baba yake kukataa asichezee Liverpool.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic