June 4, 2013




Kocha aliyemaliza muda wake na Real Madrid, Jose Mourinho amesema hakumpanga kwa makusudi kipa Iker Casillas katika mechi za kumaliza msimu.

Mourinho amesema alijua Casillas alipania kucheza mechi hiyo, lakini akamuweka nje akijua wazi mashabiki wangeshangilia sana kurejea kwake, kitu ambacho hakutaka kitokee.

„Ulikuwa ni uamuzi sahihi na nilifurahishwa na nilichofanya,“ alisema Mourinho.


Casillas aliumia siku nne kabla ya mechi hiyo, lakini akarejea mazoezini na kufanya vizuri lakini bado kocha huyo Mreno aliyekuwa na ugomvi naye hakumpanga.

Mourinho na Casillas wamekuwa katika ugomvi kwa muda mrefu hali iliyosababisha Mourinho achukue uamuzi wa kumtumia kipa wa pili Diego Lopez katika mechi zake zote zikiwemo za Ligi ya Mabingwa Ulaya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic