June 4, 2013



KIUNGO wa Barcelona, Cesc Fabregas ametamka kuwa hana mpango wa kuihama timu yake ya sasa licha tetesi kuendelea kusambaa kuwa anawaniwa na timu za Ligi Kuu England ‘Premier’.

Fabregas ambaye ni mchezaji wa zamani wa Arsenal amekuwa akiwaniwa na Manchester United na City kutokana na kutokuwa na namba ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha Barcelona.


Kiungo huyo ambaye alifunga mabao 14 katika msimu uliomalizika amesema: “Nina furaha kuichezea Barca, nataka kuendelea kubaki hapa kwa miaka mingi zaidi.”

Barcelona ililazimika kumtumia Fabregas kuwa mshambuliaji wa kati kutokana na Lionel Messi kuwa majeruhi, lakini ujio wa Neymar unamaanisha kuwa Fabregas atarejeshwa kwenye nafasi yake ya kiungo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic