June 11, 2013


Pamoja na kukaa nje bila ya kupata namba kwa zaidi ya miezi mitano sasa, mshambuliaji wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi ameanza kazi.

Okwi raia wa Uganda alicheza kuanzia mwanzo katika mechi kati ya timu yake ya Etoile du Sahel dhidi ya JSMB.


Katika mechi hiyo ya ligi Okwi hakufunga lakini ndiye aliyekuwa nyota kutokana na usumbufu mkubwa aliowapa mabeki wa timu pinzani.
Hadi mechi inaisha alifanyiwa faulo 17 na alitoa pasi ya bao ikiwa ni pamoja na kusababisha faulo ambayo baadaye iilizaa penalty.

Mabao ya Etoile yalifungwa na Mossaab Sassi katika dakika ya 26 na Jaziri katika dakika ya 81 na kupa ushindi Etoile wa mabao 2´-1 huku bao la wageni likifungwa na Med Derrag katika dakika ya 43.


Tokea ametua Tunisia, Okwi alikuwa akiwekwa benchi ingawa alishiriki mazoezi kama kawaida.
Awali ilionekana kama kutaka kumkatisha tamaa Mganda huyo lakini sasa anaonekana kupata uhakika wa namba.


Hata kama hatacheza, lakini kocha lazima atakuwa anamtupia jicho hasa kutokana na uwezo aliuonyesha katika mechi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic