June 3, 2013



 
Wakipata maelekezo kutoka kwa Adrian
Nimetua nchini Ujerumani, kwanza ninaanza na vijana wa Kitanzania ambao wako katika project maalum ya Fels na wanaendelea kujifunza mambo mengi, tutakuwa tunataarifiana kiana.

lakini bado naendelea na kozi fupi kuhusiana na soka la Ujerumani na nini kimefanya liendelee kuwa imara zaidi kwa miaka mingi huku msimu huu likitesa zaidi.


Ninapita katika klabu kadhaa zikiwemo za daraja la tatu ambazo zimenipa mwaliko, lengo ni kujifunza na kama nikipata nafasi kidogo nitakwenda Uswiss katika klabu ya Basel ambako ni mwendo wa dakika 25 kutokea hapa nilipo sasa, panaitwa Freiburg.

Kidogo baridi ni kali, lakini kiana mapambano yanaendelea na tutakuwa tukiendelea kujuzana na mambo mengine hasa makala, natupia kwenye CHAMPIONI pia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic