July 18, 2013



Azam Media Group imeingia Mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Simba Sports wenye thamani ya Sh milioni 331.

Mkataba huo utaiwezesha Azam TV kurusha kipindi katika runinga yake kitakachokuwa kinajulikana kama Simba TV.

Mkataba huo umesainiwa leo na pande zote mbili, Simba ikiwakilishwa na Mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage na Katibu Mkuu, Evodius Mtawala pamoja na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Hamisi Kilomoni.

Wakati upande wa Azam Media Group uliwakilisha na Abubakar Bakhresa ambaye ni mkurugenzi mkuu, Meneja Mkuu, Said Mohamed na Mwanasheria wake, Shani Christoms.

Katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Kibo ndani ya jengo la PSPF jijini Dar es Salaam, Simba walikabidhiwa hundi hiyo ambayo ilipokelewa na Rage.

Kabla ya hapo, Azam TV pia ndiyo imekuwa na nafasi kubwa ya kupata nafasi ya kuonyesha live Ligi Kuu Bara msimu ujao.

Azam TV ambayo itaanza kurusha matangazo yake hivi karibuni, imetenga dola milioni moja, zaidi ya Sh bilioni 1.6 ili kupata tenda hiyo ambayo ilikuwa inachuana kwa kasi SuperSport ya Afrika Kusini.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic