Kiungo
nyota wa zamani wa Manchester United, David Beckham amemshauri mshambuliaji Wayne
Rooney kuendelea kubaki OT.
Rooney
amekuwa hana raha tena katika klabu hiyo na ameshaandika barua kuomba kuondoka
lakini uongozi wa Man United pamoja na Kocha David Moyes wametaka mshambuliaji
huyo abaki.
![]() |
| BECKHAM (KUSHOTO) AKIWA NA WAKONGWE WA ENZI ZAKE WAKIWA MAN UNITED AMBAO NI SCHOLES, BUTT, GIGGS, PHILL NA GARRY NEVILE |
Wameishatangaza
kwamba Rooney hatauzwa pamoja na juhudi za Chelsea na Arsenal kuonyesha
wanamhitaji.
“Kwa
kuwa Rooney ni mchezaji mwenye kipaji cha hali ya juu, naona sehemu
anayostahili ni Manchester, hivyo itakuwa vizuri kama atakubali kubaki,” alisema.
Dalili
zinaonyesha Rooney ataendelea kubaki United lakini Kocha Jose Mourinho wa
Chelsea amekuwa akiendelea kumshawishi kwa kuzungumza kwenye vyombo vya habari
kwamba anahitaji ajiunge naye Stamford Bridge.









0 COMMENTS:
Post a Comment