July 15, 2013





Manchester United imeamua kukata mzizi wa fitina na sasa imeweka mezani pauni milioni 26 ili kumsajili kingo wa Barcelona, Cesc Fabregas.

Uamuzi huo wa United umetokana na timu hiyo kumkosa kiungo mshambuliaji mwingine Thiago Alcantara ambaye amesajiliwa na Bayern Munich.


Kocha David Moyes anataka kumuunganisha Fabregas kwa mara nyingine na Robin van Persie.

Wawili hao walicheza kwa ushirikiano mkubwa wakati wakiwa katika kikosi cha Arsenal na Fabregas ,26, alimuachia van Persie utepe wa unahodha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic