![]() |
| OLOYA AKIWA KAZINI NCHINI VIETNAM... |
Mshambuliaji
Moses Oloya wa Saigon ya Vietnam amewahakikishia Simba kwamba atatua katika
klabu hiyo.
Oloya raia
wa Uganda amewaambia Simba kuwa ameamua kujiunga na timu hiyo bila ya kujali
amekuwa akipata ofa kutoka katika timu mbalimbali za Tanzania na kwingineko.
“Oloya
amekuwa akitakwa na timu nyingi, ziko za Tanzania nay eye anaonyesha amepania
kurudi Afrika. Hivyo amezungumza na Simba na kuwaeleza kila anachotaka.
“Tayari
wamekubaliana na amekuwa akifanya mazungumzo na klabu yake ikiwezekana imuachie
mapema yaani mwezi mmoja kabla ya mkataba wake kwisha ili akiondoka Vietnam
asirudi.
“Simba wamekubali
kumlipa mshahara wa mwezi mmoja ambao atakuwa amevunja kule. Inawezekana na
Wavietnam hao pia wanaweza kukubali kwa kuwa baada ya ligi kwisha atakuwa
amebakiza mkataba wa mwezi mmoja,”kilieleza chanzo cha uhakika.
Yanga pia
imekuwa ikimuwania mchezaji huyo kutokana na ombi la kocha wao, Ernie Brandts
lakini viongozi wake wamekuwa wakijaribu kutaka kuficha kwa kuhofia kuonekana
wanamfuatilia.
Simba ndiyo
ilikuwa ya kwanza kumfuata, Yanga wakafuatia na kusababisha mshambuliaji huyo
mwenye kasi kuwa gumzo kubwa nchini.
Bado haijajulikana
katika vita hiyo nani ataibuka mshindi na kumpata mchezaji huyo kwa ajili ya
msimu ujao.









Salehe Ally namuomba sana Mwenyezi Mungu aendelee kukupa nguvu na pumzi ili uendelee kutuletea habari nzuri na za uhakika kama hizi...MSAFIRI KAGEMA.
ReplyDelete