August 7, 2013


*Timu mbili, moja ya ligi kuu zatoa macho, wakala wake  alonga LIVE na Salehjembe
Na Saleh Ally, Strasbourg, UFARANSA
Beki nyota wa Simba, Shomari Kapombe ameonyesha kweli ana kipaji baada ya kufuzu majaribio ya kucheza soka la kulipwa barani Ulaya.
Kapombe mwenye umri wa miaka 21 amefuzu kucheza soka katika timu mbili moja ikiwa inayoshiriki Ligi Kuu ya Ufaransa.

Championi ambalo linaendelea kuranda nchini Ufaransa limepata taarifa hizo za uhakika mjini hapa, lakini wakala wake Denis  Kadito ameendelea kusisitiza kuomba timu hizo ziwe siri hadi hapo atakapozungumza na Simba.

“Kweli Kapombe amefanya vizuri sana, tulimpeleka majaribio AS Cannes. Hii timu iko daraja la nne, CFA, chini ya Ligue 1, Ligue 2 na National. Sababu ya kufanya hivi ni kwamba timu za Ligue 1 zina 2nd team ambazo wanacheza ligi hiyo ya 4 pamoja na AS Cannes.

“Kwahiyo basi, kwavile idea ilikuwa tumpeleke highest division, inamaana akiweza kucheza AS Cannes, ataweza kucheza 2nd team ya Ligue 1 club. Hapa tulikuwa tuna-avoid kumpeleka moja kwa moja Bordeaux ambapo kulikuwa na uwezekano wa kumpeleka. Tukahofia kuunguza opportunity incase level yake isingefikia. Tulichofanya, kupitia washirika wenzangu Ufaransa, waliwasiliana na maScout wa Club mbalimbali za Ligue 1 kuja kumwangalia katika mechi. Na timu huwa zinakuja kutafuta wachezaji AS Cannes.

“AS Cannes ni timu kubwa sema walifanya makosa financially na management wakashuka kutoka Ligue 1 hadi hapo walipo. Hii ndio timu iliyotoa kina Patrick Viera, Zinedine Zidane na Luis Fernandes (mchezaji mkali wa 1980’s). Timu iko vizuri sana hata ukiongea na Kapombe atakueleza,” alisema Kadito, wakala kijana aliyepania kuona Tanzania nayo inapata wachezaji wa kulipwa barani Ulaya.


Taarifa zinaeleza tayari wakala huyo ameanza mazungumzo na Simba kuhusiana na Kapombe kujiunga na moja ya timu hizo za Ufaransa. Hata hivyo, umaarufu mdogo wa Tanzania katika soka huenda ukawa tatizo

Pamoja na kuwa mgeni katika soka la Ulaya, lakini Kapombe alionyesha uwezo mkubwa na kuwashangaza baadhi ya mawakala wengine ambao walialikwa kwa ajili ya kumuangalia.
Utulivu wake kwenye mpira, basi za uhakika na ujuzi wa kukaba, zilionyesha kuwavutia mawakala wengi.
Suala la Tanzania kutokuwa maarufu kisoka, huenda ndiyo limekuwa hofu kwao lakini tayari Kapombe amemaliza kazi yake, kilichobaki ni makubaliano tu katika ya klabu itakayomtaka na Simba.

Salehjembe inaendelea kuranda anga hizi huku likifuatilia zaidi kujua kuhusiana na mchezaji huyo kinda Mtanzania ambaye kama atapata nafasi, huenda akawa amewasaidia Watanzania wengine kutoka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic