Na Wilbert
Molandi
KLABU ya
Simba imeiambia Al-Markhiya Sports Club ya Qatar imalizane na Etoile du Sahel
ya Tunisia ili imsajili kiungo wake mshambuliaji, Emmanuel Okwi.
Kauli hiyo
imetolewa saa chache baada ya klabu ya Al Markhiya Sports Club iliyomnunua
kiungo mshambuliaji wa Simba, Mwinyi Kazimoto, kuonyesha nia ya kumsajili
kiungo huyo mwenye kasi.
Akizungumza
na Championi Jumatano, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya timu hiyo, Zakaria
Hans Pope, alisema kuwa kama klabu hiyo ipo tayari kutoa dola 300,000 (zaidi ya
shilingi milioni 480) izipeleke Etoile du Sahel ili imchukue Okwi.
Hans Pope
alisema, Etoile du Sahel hawana shida, hivyo wawafuate kwa ajili ya kufanya
mazungumzo, kwani bado ni mchezaji mzuri mwenye uwezo mkubwa wa kucheza soka.
“Sisi
tunasubiri fedha zetu za usajili kutoka huko Etoile du Sahel tulizomuuzia Okwi,
hatuwezi kuingilia mazungumzo, nyie kama mnamtaka wafuateni mkafanye nao
mazungumzo.
“Kikubwa
mnatakiwa kujua kuwa dau lake la usajili ni dola 300,000, zipelekeni Etoile du
Sahel ili mumchukue,” alisema Hans Pope.
Naye
mwakilishi wa Al-Markhiya Sports Club, Saleh Afif, alisema: “Tunataka
kuiimarisha timu yetu ili ipande daraja kwenye msimu ujao, tunaamini tukimpata
Okwi malengo yetu yatafanikiwa.
“Acha
tukajadiliane kwanza na viongozi kabla ya kwenda kufanya mazungumzo na Etoile
du Sahel,” alisema Afif.








0 COMMENTS:
Post a Comment