August 7, 2013



Na Joan Lema
KOCHA Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts, amewaonya vikali wachezaji wa klabu hiyo, Hussein Javu na Rajabu Zahir kwa kuchelewa kufika kwenye maandalizi ya timu hiyo kabla ya mechi ya Mtibwa Sugar wikiendi iliyopita.
Chanzo makini kutoka ndani ya klabu hiyo kilisema kuwa, mara baada ya kumalizika kwa mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Taifa na Yanga kuibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 3-1, Brandts aliwajia juu wachezaji hao kwa kuchelewa.
Kikizungumza na Championi Jumatano, chanzo cha ndani kutoka Yanga kilisema wachezaji hao walionyesha utovu wa nidhamu kwenye kikao cha kabla ya mechi kilichofanyika kwenye makao makuu ya klabu hiyo Jangwani jijini Dar es Salaam.
Chanzo hicho kilisema kuwa wachezaji hao walikuwa kwenye kikosi cha kwanza kwenye mchezo huo dhidi ya Mtibwa, lakini kutokana na kuchelewa huko, Brandts aliwaondoa na kuwafanya wachezaji wa akiba.
 “Kocha alisisitiza kuwa hatataka jambo hilo kujirudia tena, kwani hapendezwi na utovu wa nidhamu wa aina yoyote.
“Kocha alikuwa awaanzishe lakini hali hiyo ilisababisha awatoe kwenye kikosi cha kwanza, hili ni onyo, nafikiri wakirudia tena watakumbwa na adhabu kali,” kilisema chanzo hicho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic