September 26, 2013





Siku 767 baada ya kurejea Arsenal, mshambuliaji Nicklas Bendtner, jana alishindwa kufunga breki na kuivaa nguzo.


Bendtener alikuwa akiichezea timu yake ya Arsenal katika mechi ya Kombe la Capital One dhidi ya Wes Brom Albion.




Bendtner alikuwa akijaribu kuiwahi krosi ya kiungo Ryo Miyaichi ili aukwamishe mpira wavuni.

Hata hivyo alishindwa, mwisho akaivaa nguzo hiyo na kulazimika kulala chini kutokana na maumivu.



Kiburudisha zaidi kilikuwa ni mabadiliko ya mwonekano wake, kwani safari hii Mdenishi huyo alikuwa ameachia ndevu kwa wingi pamoja na nywele zake, tofauti na alivyokuwa akionekana hapo awali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic