September 27, 2013





Beki wa kati wa Simba raia wa Burundi, Gilbert Kaze ameshangazwa na soka lililoonyeshwa na Mbeya City inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara na kufika mbali akidai kuwa inao uwezo wa kutwaa ubingwa kama itaendelea na mwendo mzuri.


Kaze ambaye ametua Simba hivi karibuni, akitokea Vital’O ya Burundi na kusaini mkataba wa miaka miwili, amesema kuwa katika mechi tano za ligi hizo hajaona timu iliyoonyesha ushindani mkali kama Mbeya City ambayo imepanda daraja mwaka huu.

“Simba tumecheza mechi tano za ligi mpaka sasa, nimefurahishwa na kiwango cha Mbeya City walichokionyesha tulipocheza nao.

“Ninaamini kama mechi zote wakiendelea kucheza jinsi walivyocheza na sisi, basi wataifunga kila timu watakayocheza nayo ikiwezekana hata kutwaa ubingwa, timu yao inaundwa na vijana wengi wenye kasi,” alisema Kaze.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic