September 27, 2013


Hatimaye mshambuliaji Mrisho Ngassa amemalizana na Simba baada ya kuzikabidhi Sh milioni 45 kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), leo.

Ngassa amesema amewasilisha fedha hizo kwa TFF na Simba watalipwa na shirikisho hilo.

Ngassa aliongozana na mjumbe wa sekretalieti ya Yanga, Patrick Naggi na kukabidhi fedha hizo katika kitengo cha fedha cha Yanga.

“Kweli nimemalizana nao, sasa naelekeza nguvu zangu katika kuisaidia Yanga,” alisema Ngassa.
Ngassa alitakiwa kulipa Sh milioni 45 baada ya kuchukua Sh milioni 30 za Simba. Sh milioni 15 imekuwa ni adhabu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic