September 27, 2013





Uongozi wa timu ya Tanzania Prisons umetoa neno kwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kuwa hatakiwi kuitenga timu hiyo na kuelekeza nguvu zake kwenye kikosi cha Mbeya City pekee wakati zote ni timu za Mkoa wa Mbeya.


Katibu Mkuu wa Prisons, Sadiki Jumbe amesema kumekuwa na hali ya upendeleo kwa wenzao wa Mbeya City wakati huu ambapo Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea.

“Timu zote zipo katika jimbo lake na wote ni wapiga kura wake, hivyo tunamuomba mbunge wetu asitubague kama wananchi wanavyotutenga kwani kuna utofauti mkubwa sana kwa sapoti wanayopewa wenzetu wa Mbeya City na sisi.

“Nilidhani yeye ndiye angekuwa mstari wa mbele au kuwa mfano wa kutupa sapoti lakini (Sugu) anakuwa wa kwanza kutubagua, hii hali inatuumiza sana na inawaathiri hadi wachezaji wetu.

“Mfano mapato ya Mbeya City na Yanga yalikuwa milioni mia lakini sisi na Yanga ni milioni arobaini na nne, kwa nini inakuwa hivyo, inauma sana,” alisema katibu huyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic