September 25, 2013





Sakata la kiungo Mrisho Ngassa limechukua sura mpya baada ya kupata ofa ya Sh milioni 105.

Awali Ngassa alikuwa tayari kusaini mkataba mdogo wa maelewano na klabu ya Yanga ili alipiwe deni la Sh milioni 45 kwa Simba, naye atakuwa akikatwa Sh 500,000 kila mwezi katika mshahara wake.


Lakini sasa Ngassa ametaka apewe siku kadhaa na kutafakari kuhusiana na suala la ofa hiyo kutoka Oman.

Pamoja na uamuzi wake wa kutafakari, bado inaonekana Ngassa anabanwa na mkataba wa Yanga ambao ndiyo wenye haki naye baada ya TFF kumpitisha upande wa Jangwani na si Msimbazi.

Hivyo, hata kama akiamua kuondoka, atalazimika kuomba ruhusa ya Yanga ambao kama hawataki, atakuwa ‘ameumia’.

Habari kutoka ndani ya Yanga zimeeleza, suala hilo linashughulikiwa na lilianza kufanyiwa kazi tokea kwenye mkutano na chakula cha usiku kilichoongozwa na mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji.

Blog hii ilikuwa ya kwanza kuandika jana kuhusiana mkutano huo kwenye hoteli ya Serena.

Ngassa alionyesha kiwango kizuri akiwa na Simba msimu uliopita, kwani katika 27 alizocheza, 6 akiwa ameingia na 7 ametoka, alifanikiwa kufunga mabao saba na pasi 15 zenye macho zilizozaa mabao.

Ngassa ataungana na wenzake rasmi kesho kwa ajili ya kambi tayari kuivaa Ruvu Shooting Jumamosi na atacheza uwapo tu Yanga watakubali kumlipia deni hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic