October 9, 2013





Meneja wa Klabu ya Kagera Sugar, Mohamed Hussein, amesema pamoja na kuwepo kwa malalamiko mengi juu ya ubovu wa Uwanja wa Kaitaba ambao unatumiwa na timu yao kama uwanja wa nyumbani, bado na wao ni wageni wa dimba hilo kwani huutumia siku ya mechi tu.


Uwanja huo unaomilikiwa na Manispaa ya Bukoba, unadaiwa kuwa miongoni mwa viwanja vibovu Tanzania vitumikavyo kwenye ligi kuu na kudaiwa kuwa chanzo cha matokeo mabaya kwa timu ngeni.

Akizungumza na Championi Jumatano, Hussein alisema Kagera Sugar huutumia siku ya mechi tu kwani kuna uwanja wenye hadhi zaidi ya Kaitaba ambao wanautumia kwenye mazoezi na maandalizi ya mechi mbalimbali.

“Pale (Kaitaba) na sisi ni wageni. Tunautumia wakati wa mechi tu, maana maandalizi ya mchezo wowote huwa tunafanyia kwenye uwanja wetu wa Kagera A, uliopo Misenyi wakati Kaitaba upo Bukoba,” alisema Hussein.

Aliongeza kuwa, Kagera A una kiwango kizuri zaidi ya Kaitaba, lakini tatizo lake haujatimiza masharti ya Fifa, likiwemo la kukosa uzio (fensi) na kusema wameanza mradi wa kuboresha uwanja wao ili kuachana na Kaitaba msimu ujao.

Tayari kikosi cha Kagera kimeingia kambini kujiwinda na mchezo wa Jumamosi dhidi ya Yanga utakaopigwa kwenye uwanja huo wa Kaitaba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic