October 7, 2013




Inawezekana kabisa kiungo mkongwe zaidi wa Manchester United, Ryan Giggs ataweka rekodi itakayokaa muda mrefu zaidi katika ligi hiyo.
 
Hadi sasa anaongoza kwa kucheza mechi 620 za Premiership, anayemfuatia ni kipa wa zamani wa Liverpool na Portsmouth, David James, mwenye 572.

Frank Lampard wa Chelsea ana mechi 552 na ndiye pekee anayeweza kufikia rekodi ya Giggs kwa kuwa bado anaendelea kucheza katika ligi hiyo ingawa inaonyesha anahitajika kudumu kwa zaidi ya misimu mingine minne.

Katika idadi ya wachezaji wenye mechi nyingi, ndani ya 10 bora ni Giggs na Lampard tu ndiyo wanaoendelea kucheza hadi leo.

Maana yake kufikia rekodi ya mkongwe huyo haiwezi kuwa kazi rahisi. Giggs ana miaka 39 na alianza kucheza ligi hiyo kwa mara ya kwanza katika msimu wa 1990-91.

10 BORA YA WALIOCHEZA MECHI NYINGI:
1       Ryan Giggs  620
2       David James  572
3       Frank Lampard  552
4       Gary Speed  534
5       Emile Heskey  517
6       Jamie Carragher  508
7       Phil Neville  505
8       Mark Schwarzer  504
9       Sol Campbell  503
10     Gareth Barry  500

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic