October 13, 2013






Inawezekana kabisa kipindi cha wiki moja kuanzia leo, ndiyo huwa kigumu zaidi kwa vikosi vya Yanga na Simba.

Timu hizo mbili zimekuwa na hofu kubwa mara tu zinapomaliza mechi ya mwisho kabla ya ile dhidi ya wao.


Baada ya Simba kumaliza dhidi ya Prisons na kushinda 1-0, Yanga nao dhidi ya Kagera Sugar na kuilaza 2-1, sasa macho kwa watani.
Kila upande unatawaliwa na hofu na lawama zinaanza kwa kila mtu anayepita mbele yao.

Hofu huwa kubwa kwa zaidi ya asilimia 120, kila upande ukitupa jicho upande wa pili lakini ukifanya ulinzi mkubwa upande wake.
Hakuna mechi kati ya timu hizo imewahi kukaribia bila ya pande hizo mbili kutuhumiana katika hujuma.

Yanga wanaamini Simba watafanya hivyo, Simba vivyo hivyo.
Lakini hata ndani ya klabu hizo, wao wenyewe hawaaminiani kwa kuwa kila mmoja anaona kama mwenzake anamuuza.

Hii inatokana na makundi ambayo yamo kila upande wa klabu moja.
Kundi lililo madarakani linakuwa na hofu, kwamba litahujumiwa hivyo, Simba hawawaamini Simba na Yanga hawawaamini Yanga.
Kazi katika mechi hiyo inakuwa kubwa zaidi kwa kuwa kila upande unautuhumu mwingine lakini unajituhumu wenyewe.

Halafu siku ya mwisho, mechi hiyo inamalizika kwa dakika 90 za kawaida kama ambavyo inaweza kuwa mechi ya Kagera Sugar au Prisons.

Undugu au urafiki wa watu wengi wa Yanga na Simba, kipindi hiki huzorota na wengi hukwepana.

Wako wanaohofia kuzungumza na wengine kwa kuwa wataonekana wamesaliti hasa kama timu itatokea ikafungwa.

Lakini kuna kichekesho zaidi, kama ikitokea timu moja ikafungwa, hakuna anayeona ni matokeo ya uwanjani, lazima mzigo uangushiwe kwa mtu au watu fulani.

SIMBA, YANGA, BADILIKENI KWA KUWA MNAISHI KATIKA KARNE YA 17. TIMU ZENU ZINAWEZA KUSHINDA AU KUSHINDWA BILA YA KUWA NA HUJUMA.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic