October 6, 2013





Mshambuliaji nyota wa Simba, Amissi Tambwe amesema yeye ni muumini wa dini ya Kikristo tokea kuzaliwa kwake ndiyo maana alionyesha ishara ya msalaba baada ya kufunga bao.


Tambwe raia wa Burundi ameiambia blogu hii kwamba jina la Amissi limekuwa likiwachanganya wengi, lakini ni la ukoo na alipewa akiwa mdogo.

“Hili ni jina langu tokea nikiwa mtoto, watu wamekuwa wakilichanganya sana na wanadhani ni Muislamu, lakini hapana,” alisema.

Mkanganyiko wa kuwa Tambwe ni muumini wa dini gani baada ya kufunga bao lake la nane katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, jana.

Baada ya kufunga bao hilo, Tambwe alionyesha ishara ya msalaba, hali iliyoonyesha kuwachanganya wengi waliokuwa wakiamini ni Muislamu.
Tambwe amefunga mabao nane katika mechi sita za Ligi Kuu ya Vodacom na ndiye anaongoza kwa wapachika mabao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic