October 7, 2013





Uongozi wa Lipuli inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, imesema bado inaamini Shadrack Nsajigwa ni kocha wao.


Nsajigwa, hivi karibuni aliripotiwa kutangaza kuitosa timu hiyo kutokana na kushindwa kuwajali wachezaji wake.

Katibu Mkuu wa Lipuli, Wile Chikweo, amesema wanashangazwa na taarifa zilizoenea kuwa Nsajigwa ameikimbia timu hiyo.

Amesema wao wanajua yupo nyumbani kutokana na matatizo ya kifamilia na hajawajulisha kuhusu kuachana na kazi.

 “Tumekuwa tukisikia kwenye vyombo vya habari kuwa Nsajigwa kaondoka, sisi bado tunamtambua kama kocha wetu, maana ana mkataba wa maandishi, hatujavunja mkataba wake.

“Aliomba ruhusa kwenda kumuuguza mama mzazi, akisema hakuwa na muuguzi, mpaka leo (jana) hajatutaarifu chochote kuwa ameachia ngazi,” alisema katibu huyo.

Kabla ya Nsajigwa kutangaza kuachia ngazi, Lipuli ilikuwa imepoteza michezo mitatu mfululizo ya Ligi Daraja la Kwanza na nyota huyo wa zamani wa Yanga akasema timu haiwezi kufanya vizuri kwa kuwa haiwajali wachezaji wake, hivyo ameamua kujiweka kando.

Kwa sasa timu hiyo ipo chini ya kocha Fide Kalinga ambaye anakaimu na wiki iliyopita aliiongoza kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Majimaji.

Nsajigwa alipotafutwa na Championi Jumatatu jana simu yake ilikuwa ikiita kwa muda mrefu bila kupokelewa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic