October 9, 2013





Baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kudai limemuomba radhi mshambuliaji wa kimataifa wa Simba, Amissi Tambwe raia wa Burundi straika huyo ameibuka na kudai ni waongo.


Tambwe alifunga mabao manne katika mchezo dhidi ya Mgambo Shooting, Septemba 18 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa na kunyimwa mpira kama zawadi baada ya mechi kumalizika.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura amesema wamemuomba radhi straika huyo kutokana na kutopewa mpira huo licha ya kuwa suala hilo halipo kwenye sheria za Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).

Alisema waliamua kumuomba radhi kama ‘fair play’ lakini walimtaarifu aufuate  katika ofisi za shirikisho hilo na pia mwamuzi aliyemnyima mpira huo hawezi kuadhibiwa.

“Tulimuomba radhi kutokana na tukio lile na tulimtaka aje kuchukua mpira wake nafikiri atakuwa anajipanga ili aje kuchukua siku yoyote,” alisema Wambura.

Championi lilienda mbele na kumtafuta straika huyo anayeongoza kwa kufunga mabao kwenye ligi kuu kwa sasa akiwa ameshatupia nane wavuni ambapo alidai  hajafuatwa na mtu yeyote kuhusiana na suala la kupewa mpira na hafikirii tena suala hilo.

“Sijafuatwa na mtu yeyote na wala sina wazo lolote kuhusiana na ishu hiyo ya mpira na kama wataamua wenyewe kuniletea au wakiukabidhi kwa viongozi wangu sawa tu nitauchukua,” alisema Tambwe na kuongeza:
“Naumwa maralia tokea jana na sijfanya mazoezi  yoyote kwa kuwa mwili unaniuma sana.” 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic