October 12, 2013


England imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Montenegro katika mchi yao ya kuwania kucheza Kombe la Dunia nchini Brazil, mwakani.

Katika mechi hiyo iliyopigwa kwenye Uwanja wa Wembley na kumalizika hivi punde, mabao ya England yalifungwa na Wayne Rooney, beki wa Montenegro akajifunga, kinda Townsend akapiga la tatu kabla ya Sturridge kujiangusha na kupata penalty aliyoikwamisha wavuni.

LUKAKU AKIFUNGA BAO LA KWANZA, MABAO YAKE YAMEIPELEKA UBELGIJI KWENYE KOMBE LA DUNIA


Wakati England inashinda mabao hayo, Sweden ikiwa nyumbani ililazimika kusubiri hadi dakika ya 86 kupata bao la pili na la ushindi lililofungwa na Zlatan Ibrahimovic.

Mechi hiyo dhidi ya Austria ambayo pamoja na kuwa wageni walitangulia kupitia Martin Hank, Martin Olsson akasawazisha na Zlatan akamaliza kazi.
MODRIC NA HAZARD WAKIWANIA MPIRA

HAZARD KAZINI...

Upande mwingine, Uholanzi imeishindilia Hungry kwa mabao 8-1 huku mshambuliaji wa Manchester United, Robin van Persie akipiga mabao matatu yaani Hat trick. Mabao mengine ya wenyeji yalifungwa na Strootman, Jeremain Lens, van der vaart na Arjen Robben.

Ujerumani nayo ikaichapa Ireland kwa mabao matatu huku Sami Khedira, Andre Schurrle wa Chelsea na Mesut Ozil wa Arsenal wakipachika mabao hayo matatu.

Urusi wakiwa ugenini wakaiangusha Luxembourg kwa mabao 4-0. Slovenia ikaiagunia Norway kwa 3-0, Iceland ikaitandika Cyprus 2-0 na Uturuki ikicheza ugenini ikashinda 2-0 dhidi ya wenyeji Estonia.



Italia ikiwa ugenini imelazimisha sare ya 2-2 dhidi ya Denmark, Coratia ya kina Modric imelala nyumbani 2-1 dhidi ya Ubelgiji na Romelu Lukaku ndiye muuaji aliyepiga zote na kuipa timu yake ya taifa nafasi ya kwenda World Cup. Mara ya mwisho, Ubelgiji ilicheza michiano hiyo mwaka 2002 ilipofanyika Japan na Korea Kusini.

Wales ya kina Bale ikailamba Macedonia 1-0 na Jamhuri ya Czech ikaipindua Malta kwa kuichakaza kwa bao 4-1.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic