Rasmi leo msanii maarufu wa hip hop, Afande Sele
amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Afande ameonyesha ni mwenye furaha na kwenye mtandao wa
Facebook ameweka maneno haya.
Hakuna kusanda,hakuna
kumbwanda,mbele kwa mbele makamanda,vua gamba vaa gwanda kisha kaza mkanda,
wanashuka sisi tunapandaaa,,,,Leo tunaanza kuandika hisyoria mpya ktk mkoa wetu
wa morogoro na tz kwa ujumla kwa sababu nikiwa kama msanii wa muda mrefu na
mfalme pekee wa mzk wa kizazi kipya ninaetunga nyimbo zangu kwa kuzingatia
ujumbe muhimu ktk jamii kwa mambo ya kisiasa,kiuchumi,elimu,amani na upendo nk,sasa leo nimeamua kwa ridhaa yangu iliyosukumwa na uzalendo na
mapenz makubwa kwa taifa langu kuchukua kadi ya kujiunga rasmi uanachama wa
CHADEMA,tukio hilo kubwa litafanyika leo jioni ktk mkutano wa hadhara
utakaofanyika kata yetu ya mafiga/misufini na utahudhuriwa na viongoz
mbalimbali wa chama kutoka makao makuu ya chama dsm pamoja na mbunge wa
nyamagana mh ezekiel wenje,kwa wakaz wa moro wazalendo nyote mnakaribishwa
saaana,ahsanteni wana'ndugu,siasa si uadui,tupingane/ tusipigane,Pendo moja!
Dalili za kushindwa kasi ya vijana kwenye muziki wa bongo na Hip pop ndio imewakimbiza wakongwe wa muziki huo na kwenda kwenye siasa lakini anguko la maisha huenda likaanzia hapo maana shida ni ubunge tu.
ReplyDeleteEmma James