Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky
Maxime amesema Simba wamefainika kumnasa kiungo, Awadhi Juma.
Simba imesamsajili Juma kwa mkataba wa
miaka miwili na mzunguko wa kwanza katika Ligi Kuu baraaliichezea Mtibwa Sugar.
“Kweli Simba wamepata mchezaji mzuri
sana, jamaa anajituma na ana uwezo pale katika kiungo. Lakini itategemea
wanamtumia vipi,” alisema.
Pamoja na kiungo huyo, Simba
imemsajili mshambuliaji Ally Badru Ally aliyekuwa anakipiga katika klabu ya Canal Suez ya Misri.
Wote wawili wameanguka mkataba wa
miaka miwili kwa Simba na wataanza kuonekana na timu hiyo katika mechi za
kujiandaa na mzunguko wa pili.
0 COMMENTS:
Post a Comment