Wakati burudani ya Ligi Kuu England ikiendelea, pamoja na ushabiki wa timu kubwa au
maarufu kama Arsenal, Manchester United, Chelsea na Manchester City kuwa
kipaumbele, lakini zinaonekana kufeli katika mambo kadhaa.
Ikiwa ni kila
baada ya timu kucheza mechi 11, inaonekana Aston Villa ambayo imekuwa
ikiwashangaza wengi msimu huu, ndiyo timu yenye ngome ngumu zaidi.
Katika mechi
hizo 11, Southampton imeruhusu mabao matano kutinga katika nyavu zake, hali
ambayo imeisaidia kuwa katika tano bora na inashikilia nafasi ya tatu ikiwa na
pointi 22.
Angalau
Arsenal, Chelsea na Liverpool ambazo pia ziko katika tano bora zimeonyesha kuwa
na ngome nguvu, tena zinazofanana kwa mwendo, kwani zote zimeruhusu mabao 10
katika mechi hizo 11.
Manchester
United inayoshika mkia katika tano bora, bado inaonekana kutokuwa imara sana
kwani katika mechi hizo 11, imeruhusu nyavu zake kutikiswa mara 13.
Lakini hilo
si suala kubwa sana, ishu zaidi ni katika takwimu za kila mechi, kwamba timu
ilicheza bila ya kufungwa hata bao moja ‘clean sheet’, hii ni bila ya kujali
imeshinda au kufungwa.
Timu kubwa au
maarufu kama Man United, Arsenal na Chelsea zimefeli kwa kiasi kikubwa kwa kuwa
na ngome ambayo inaweza kuizuia timu nyingine kumaliza mechi bila ya kufungwa
hata bao moja.
Katika mechi
11 zilizocheza, timu hizo zimetoka katika mechi tatu tu bila ya kufungwa bao
hata moja, hivyo kuzifanya zishike nafasi ya chini ya kuwa timu zinazoaminika
kwa kuwa na ngome ngumu yenye uhakika wa kuzuia nyavu zake kutoguswa kabisa.
Ubora wa
ngome wa timu hizo tatu katika suala la kuzuia kutofungwa hata bao moja kwa
kila mechi zinazocheza ni 27.3%, wastani ambao unashika nafasi tatu za chini.
Crystal
Palace na Sunderland ambazo ziko mkiani mwa ligi hiyo, ndiyo timu ambazo zina
uwezo mdogo kabisa wa kuzuia zisifungwe hata bao moja kwa mechi zinazocheza.
Katika mechi 11, zilitoka uwanjani bila ya kufungwa hata bao moja katika mechi
moja tu ambao ni wastani wa 9.1% na ndiyo wa chini kabisa.
Fulham
inafuatia, inashika nafasi ya pili kwa wastani mbaya wa clean sheet, katika
mechi 11, ni mbili tu haikufungwa hata bao moja na ina wastani wa 18.2.
Ingawa
inashika nafasi ya saba katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 20 ambazo ni
sawa na zile za Man United na Everton, Tottenham ndiyo timu inayomiliki ngome
ngumu zaidi kwa kuwa katika mechi 11, imecheza 7 bila ya kuruhusu hata bao moja
na wastani wake wa ubora ni 63.5%.
Southampton,
Everton na West Ham ndizo zinazoshika nafasi ya pili kwa ubora wa kutoruhusu hata
bao moja katika kila mechi, kwani katika 11 zilizocheza, zilitoka uwanjani mara
sita nyavu zao zikiwa hazijaguswa. Wastani wao ni 54.5%.
Katika
vigogo, Liverpool inaungana na Aston Villa, Newcastle Utd, Manchester City,
Swansea City na Wes Brom kwa kuwa timu
yenye wastani wa 36.4% kwa kucheza mechi 11, kati ya hizo zikatoka uwanjani
mara nne bila ya kufungwa hata bao moja.
Katika soka
pointi ndiyo suala muhimu la kwanza, baada ya hapo unaangaliwa wastani wa mabao
ya kufunga na kufungwa. Maana yake timu ambazo zinaweza kucheza mechi bila ya
kufungwa hata bao moja, zinakuwa na uhakika katika wastani mzuri wa mabao ya
kufunga na kufungwa ambao ni muhimu.
Mara nyingi
hutokea timu zikalingana pointi, iliyokuwa makini katika kutoruhusu ngome yake
kutikiswa kirahisi inakuwa na nafasi ya kuwa juu ya nyingine ambayo haikuwa na
ngome imara au hesabu bora za kuruhusu mabao.
Kimahesabu,
makocha Arsene Wenger, Jose Mourinho na David Moyes wapo katika changamoto kwa
kuwa Liverpool, Tottenham, Southampton na Manchester City zinaweza kuwasumbua
baadaye kama itatokea wakalingana mabao ya kufunga.
CS
|
Pld
|
Perc.
|
|
7
|
11
|
63.6%
|
|
6
|
11
|
54.5%
|
|
6
|
11
|
54.5%
|
|
6
|
11
|
54.5%
|
|
4
|
11
|
36.4%
|
|
4
|
11
|
36.4%
|
|
4
|
11
|
36.4%
|
|
4
|
11
|
36.4%
|
|
4
|
11
|
36.4%
|
|
4
|
11
|
36.4%
|
|
4
|
11
|
36.4%
|
|
3
|
11
|
27.3%
|
|
3
|
11
|
27.3%
|
|
3
|
11
|
27.3%
|
|
3
|
11
|
27.3%
|
|
3
|
11
|
27.3%
|
|
3
|
11
|
27.3%
|
|
2
|
11
|
18.2%
|
|
1
|
11
|
9.1%
|
|
1
|
11
|
9.1%
|
0 COMMENTS:
Post a Comment