Kesho ndiyo jibu sahihi kwa uongozi wa Simba, kwamba utalibakiza benchi la ufundi la Simba au utafanya mabadiliko.
Bado Makocha Abdallah Kibadeni na msaidizi wake, Jamhuri Kihwelo 'Julio' wamekuwa wakijadiliwa kutokana na mwenendo wa timu hiyo.
Lakini kama wataporteza mchezo wa kesho ambao ni wa mwisho wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ashanti, basi kutakuwa na matatizo.
Kwa ujumla, mechi za kukamilisha mzunguko wa
kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zinaanza kesho (Novemba 6 mwaka huu) ambapo
Ashanti United itakuwa mwenyeji wa Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Viingilio katika mechi hiyo
itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili chini ya mwamuzi Andrew Shamba kutoka Pwani
ni sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Waamuzi wasaidizi ni
Abdallah Mkomwa na Rashid Abdallah wote kutoka Pwani wakati mezani atakuwa Hamisi
Chang’walu.
Mechi nyingine za kesho ni JKT Ruvu
Stars na Coastal Union (Uwanja wa Chamazi), Kagera Sugar na Mgambo Shooting
(Uwanja wa Kaitaba, Bukoba) na Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar (Uwanja wa
Manungu, Morogoro).
Keshokutwa (Novemba 7 mwaka huu)
raundi ya 13 kumaliza mzunguko wa kwanza itakamilika kwa mechi kati ya Yanga na
Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh.
15,000 na sh. 20,000.
Azam itakuwa mwenyeji wa Mbeya City
kwenye Uwanja wa Chamazi wakati Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora
utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Rhino Rangers na Tanzania Prisons kutoka
Mbeya.
Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza
na Mbeya City, Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam wakati Rhino itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons.
0 COMMENTS:
Post a Comment