Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts amemuweka kando
beki wake David Luhende ili afanye mazoezi pekee.
Luhende amewekwa kando kutokana na kuwa na maumivu
na Brandts amemtaka afanye mazoezi pekee. Awali Luhende alianza mazoezi pomoja na wenzake lakini baadaye Brandts akamtoa na kumtaka akimbie peke yake.
Wakati wenzake walikuwa wanafanya mazoezi pamoja,
Luhende aliendelea kuzunguka uwanja taratibu.
Brandts alimtaka Luhende kufanya mazoezi ya pekee
wakati wakiendelea na mazoezi hayo kwa kuwa alikuwa hajapona vizuri.
“Bado hajapona vizuri, hivyo hatakiwi mazoezi ya
kugongana na wenzake,” alisema Brandts katika mazoezi ya Yanga kwenye Uwanja wa
Kijitonyama jijini Dar.
0 COMMENTS:
Post a Comment